Mwanamuziki maarufu wa Tanzania, Diamond Platnumz, amevunja ukimya kuhusu kuondoka kwa wasanii wake watatu wakubwa—Harmonize, Rayvanny na Mbosso—kutoka lebo yake ya WCB Wasafi. Diamond ameeleza sababu za tofauti za kuondoka kwa kila msanii na kueleza msimamo wake kuhusu mikataba ya lebo hiyo.
Mbosso: Kuondoka kwa Amani Bila Malipo
Mbosso, ambaye alijiunga na WCB mwaka 2017, ameondoka lebo hiyo kwa makubaliano ya amani bila kulipa ada yoyote ya kuvunja mkataba. Diamond alieleza kuwa uhusiano mzuri na heshima waliyojengeana ndiyo sababu ya kumruhusu Mbosso kuondoka bila malipo. Alisema:
Harmonize: Kuondoka kwa Malipo ya Tsh 500 Milioni
Harmonize, aliyekuwa msanii wa kwanza kusainiwa na WCB mwaka 2015, aliondoka mwaka 2019 baada ya kulipa Tsh 500 milioni (takriban Ksh 25 milioni) kuvunja mkataba wake wa miaka 10. Alidai kuwa mkataba huo ulikuwa wa kinyonyaji, kwani lebo ilichukua asilimia 60 ya mapato yake, hata baada ya kujitegemea kifedha katika miradi yake.
Rayvanny: Kulipa Tsh 1 Bilioni Kuvunja Mkataba
Rayvanny aliondoka WCB mwaka 2022 baada ya kulipa Tsh 1 bilioni (takriban Ksh 50 milioni) kuvunja mkataba wake wa miaka 10. Alitaka kujitegemea na kuendeleza lebo yake ya Next Level Music. Ingawa alilazimika kulipa kiasi kikubwa, aliondoka kwa heshima na kuendelea kuwa na uhusiano mzuri na Diamond.
Msimamo wa Diamond Kuhusu Asilimia 60 ya Mapato
Diamond amejitetea kuhusu sera ya WCB ya kuchukua asilimia 60 ya mapato ya wasanii wake, akisema kuwa fedha hizo hutumika kugharamia usimamizi, matangazo, na uzalishaji wa kazi za wasanii. Alisema:
Mabadiliko ya Mtazamo kwa Wasanii Wanaondoka
USemi wako ni gani