Chelsea vs Manchester City: Mtihani Mkubwa kwa Enzo Maresca Dhidi ya Mabingwa wa Ligi Kuu
Sports
Published on 18/08/2024

Chelsea inakutana na Manchester City katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza, huku Erling Haaland na Cole Palmer wakiwa miongoni mwa wachezaji watakaonza. Manchester City, mabingwa wa ligi, wanaanza harakati za kutetea taji lao kwa mara ya tano mfululizo dhidi ya Chelsea inayosimamiwa na kocha mpya, Enzo Maresca. Ingawa walipata ushindi dhidi ya Manchester United katika Community Shield, City wamekumbwa na changamoto baada ya Oscar Bobb kuumia na Julian Alvarez kuuzwa Atletico Madrid. Chelsea, chini ya kocha Maresca, wanakutana na changamoto kubwa katika mechi hii ya kwanza, lakini wana fursa ya kujaribu mbinu mpya wakiwa na nyota mpya, Pedro Neto.

Written By: Boniface Ziro

 

Comments
Comment sent successfully!

Chat Online