UTABIRI WA HALI YA HEWA.
By Dayo Radio
Published on 19/03/2026 17:18
News

Mvua kubwa inatarajiwa kuendelea kuongezeka kote nchini kuanzia tarehe 19 hadi 24 Machi 2026, huku ikifikia kilele kati ya tarehe 20 hadi 23 Machi. Kaunti ya Mombasa ni miongoni mwa maeneo yaliyo katika hatari, yakitarajiwa kupokea mvua kubwa zinazoweza kuzidi milimita 20 ndani ya saa 24.

Hali hii inaweza kusababisha mafuriko ya ghafla, kujaa kwa maji katika maeneo ya chini na kupungua kwa mwonekano barabarani.

 

 Wakazi wametahadharishwa kuwa mafuriko yanaweza kutokea hata katika maeneo ambayo hayajapokea mvua nyingi kutokana na maji yanayotiririka kutoka maeneo ya juu.

 

Wananchi wameshauriwa kuepuka kutembea au kuendesha magari kwenye maji yanayotiririka, kujiepusha na kingo za mito na mabondeni, pamoja na kutokujikinga chini ya miti wakati wa radi na dhoruba. Pia wanapaswa kulinda mali zao, kuhamisha vitu muhimu sehemu za juu na kuwa tayari kuhama hasa kwa wanaoishi katika maeneo yanayokumbwa na mafuriko mara kwa mara.

 

Mamlaka imetoa wito wa kuahirisha safari zisizo za lazima katika kipindi hiki, kufuatilia taarifa rasmi kutoka Kenya Meteorological Department na serikali ya Kaunti ya Mombasa, pamoja na kuripoti matukio ya dharura mara moja.

 

Wananchi wote wanahimizwa kuchukua tahadhari na kuweka usalama wa maisha kuwa kipaumbele.

Comments
Comment sent successfully!