NYORO AVULIWA MAMLAKA
News
Published on 13/03/2025 by Dayo Radio

URAFIKI wa kisiasa ambao ulinawiri kati ya Rais William Ruto na Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro kabla, wakati wa kampeni na baada ya Kenya Kwanza kuingia mamlakani ulionekana kufikia kikomo rasmi jana mbunge huyo alipopokonywa wadhifa alioshikilia Bungeni.

 

Bw Nyoro alivuliwa uenyenyekiti wa Kamati yenye ushawishi ya Bajeti na Ugavi (BAC) ya Bunge la Kitaifa, huku harakati za kuwaondoa wabunge wanaomuunga mkono aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kutoka uongozi wa kamati za Bunge zikichukua mkondo mpya.

 

Kufikia wakati mchakato wa kumuondoa Gachagua ulianzishwa mwaka jana, Bw Nyoro na Rais Ruto walikuwa marafiki na hata wakati mmoja jina la mbunge huyo lilitajwa miongoni mwa waliofikiriwa kurithi Gachagua kama naibu rais.

Comments
Comment sent successfully!

Chat Online