NI KUBAYA!!!!
News
Published on 23/01/2025

Shirika la kutetea haki za kibinadamu la MUHURI nchini lamtaka Waziri wa huduma za umma serikalini justin Muturi na Inspekta Mkuu wa  polisi Douglas Kanja  kujiuzulu mara moja.

 

Akizungumza na waandishi wa habari Afisa mkuu wa dharura  katika shirika hilo  Francis Auma  ametaja hatua ya waziri Muturi ya kususia mkutano wa baraza la mawaziri  kama  ukiukaji mkubwa sheria za nchini.

Auma aidha amesema huenda  Muturi  amesalia  solemba na mwenye Upweke kwenye baraza la mawaziri  baada ya kuibua madai ya utekaji nyara kwa mwanawe .

 

"Mimi naonelea Muturi angejiuzulu tu haiwezekani wewe ulichaguliwa kuwa waziri na kila wakati uwe kinyume na wenzako wakati wakenya wanahitaji huduma za kuwasaidi"

 

Vile vile ameweza kuwasuta Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja Mkuu wa kitengo cha Ujasusi Noordin Haji na mkuu wa DCI nchini Mohammed Amin   na kushinikiza watatu hao wajiuzulu kwa kushindwa kuthibiti visa vya utekaji nyara nchini.

NA HARRISON KAZUNGU.

 

 

Comments
Comment sent successfully!

Chat Online