Dikson Ndiema aliyekuwa mume wake Rebecca Cheptegei Aaga dunia
News
Published on 11/09/2024

Mwanamume kwa jina Dickson Ndiema anayedaiwa kumchoma moto mwana Olimpiki wa Uganda Rebecca Cheptegei na kusababisha kifo chake, amefariki katika hospitali ya Eldoret.

 

Ndiema alikuwa akipokea matibabu baada ya kuchomeka asilimia 41 anadaiwa kufariki baada ya kushindwa kupumua.

 

Ikumbukwe kuwa Ndiema anadaiwa kumvamia  mkewe kwa kumwagia petroli na baadae kumchoma huko Trans Nzoia.

 

Mwili wa Cheptegei unatarajiwa kuzikwa siku ya Jumamosi nyumbani kwao  Kapkoros nchini Uganda.

Comments
Comment sent successfully!

Chat Online